Home Ads

THE MILLIONAIRE CODE

MAMBO 20 NILIYOJIFUNZA KUTOKA KITABU CHA THE MILLIONEIRE CODE BY PAUL B. FARRELL.

Si kila mtu amezaliwa na asili ya kuweka akiba , na kuwekeza na kuwa na Mafanikio  wengine mafanikio kwao si alama ya fedha , Cheo , Nafasi ya juu._

Mwanagenzi Michael The Great one.

__________________________________________________________________

 

Mwandishi anaibua jambo la ajabu sana ambalo wengi wetu limekuwa jambo linalotuzuia kuyafikia mafanikio tuyatakayo, nalo si jingine bali ni kufikiri kuwa njia aliyoitumia yule na kupata mafanikio yaweza kukutoshea na wewe kuwa mwenye mafanikio, jambo ambalo ni uongo na wengi limewafanya kufanya maamuzi ya hovyo ya kiuwekezaji na kushindwa kwa kukata tamaa na kuishia njiani.

 

Kitabu hiki bora kinakuja na msingi mkuu wa wewe pia kufanya maamuzi ya kuelekea utajiri wako kulingana na kutokana njia yako inayokufaa.

1.     Jambo muhimu kwenye mafanikio yoyote unayoyataka, ni kwa kuanza kwanza kujitafuta wewe na kujifahamu na ukisha jifahamu vyema utaona mwili wako unafuata matendo ya kutengeneza utajiri bila kuchoka ama kukata tamaa.

 

2.   Unahitaji kukua sana kihisia ili uwe na uwezo wa kujitawala kihisia ,hapo ndiyo utakuwa kwenye mwelekeo wa njia nyoofu, udhaifu wa kutawala hisia zetu ndiyo jambo linalowatumbukiza wengi kwenye umaskini.

3.   Furaha na mafanikio yapo kwenye ngazi ya kujifahamu wewe na huko utakuwa na funguoa za kujifungua yaani (Codes) zako , ili kuchukua njia sahihi inayokufaa.

 

4.   Ugumu wa jambo la ya kuyafikia mafanikio haupo kwenye kuanza jambo fulani, bali tatizo kubwa lipo kwenye kufahamu njia sahihi ya kuiendea , maana unaweza kuanza na njia mbovu isiyokuwa yako na ukaja kugundua muda umeshakwenda.

 

5.    Pamoja na wataalamu wengi kufundisha njia na mbinu mbalimbali  za kupata mafanikio lakini bado kiwango cha chini cha matajiri yaani watu wanne kati ya watu milioni mia mbili , tatizo ni kuwa ushauri unaotolewa wataalamu wanafikiri kuwa kila mmoja utamfaa jambo ambalo si kweli. Vyema kutafuta njia na ushauri unaoendana na wewe ili ukufae.

 

 

6.   Epuka mtego wa kuwa na taarifa zilizopitiliza kuhusiana na mwelekeo wa kuwa tajiri, kuwa na taarifa zilizo nyingi bila kufahamu ipi inafanya kazi kwa usahihi ni sawa na kazi bure.

 

7.    Epukana na tabia ya kuyakubali na kujifunza mambo unayoyafahamu tu na yale usiyoyajua unayaacha na kuyapuuza huko ndiko kunakokuzuia kufanya mabadiliko muhimu kwenye maisha yako.

 

8.   Asilimia 90% ya watu wanaofanya maamuzi ya kufanya uwekezaji hufanya uwekezaji kwa njia zisizo sahihi kabisa na hubaki kwenye majuto ya daima.

 

9.   Makampuni mengi yanayowashawishi watu kufanya uwekezaji kwenye eneo fulani, mengi hutumia gharama za juu sana za matangazo na kuwahadaa watu ili yajipatie fedha zao na kutajirika.

 

10.                      Mara zote usiogope kuwa wa tofauti na kubali kuwa wewe ni wa kitofauti kabisa, fanya mambo yako kwa utofauti kwakua kila kitu kwako ni cha kitofauti kama:-

 

a)   Gene

b)  Vinasaba

c)   Na njia yako pia itakuwa ya kitofauti.

11.Kujifahamu na kujijua wewe ndiyo jambo lililoandikwa kwa miaka mingi sana zaidi ya miaka elfu tano iliyopita na ndugu wa Lao Tzu kwenye kitabu chake cha Tao Te Ching, na limelejewa na wanafalsafa wakubwa kama Plato aliyesema Know Thyself , basi na kwako pia jifahamu, wewe na kuwa wewe.

 

12.                       Kama unapata wakati mgumu , jifunze kujisikiliza ndani yako kuna sauti inayokwambia wewe ulivyo , sikiliza kwa umakini mzuri.

 

13.                       Anza leo kukaa darasani , ujifunze kuwa milionea na kutafuta Njia yako ya kuelekea utajiri wako na hakikisha unayapuuza haya:-

a)   Usiwasikilize wengine wanasemaje kukusu wewe?

b)  Usikazie fikra kwenye kazi ya miaka mingi uliyofanya.

 

14.                       Fanya mabadiliko makubwa kwenye maisha yako ili usiishie kwenye aina ya  maisha haya:-

i)Maisha yenye furaha bila fedha za kutosha.

ii)Maisha yasiyo na furaha bila fedha.

iii)Maisha yasiyo na furaha na una fedha.

 

15.                       Ili kushika usukani wa Maisha yako , ondoa visababu, na hapo utaona mambo yakitimia , wacha kujiambia Mimi sina msaada.

 

16.                       Hatua za mafanikio huja pale , unapoamua kubadilika , bila kubadilika utajichelewesha wewe mwenyewe.

 

17.                       Hizi ndiyo njia ambazo huwa unatumia kufanya maamuzi yako mbalimbali kwenye Maisha yako kuwa Nazi umakini:-

 

i)Hisi (Sensation) hizi husema kitu kipo

ii)Kufikiri (Thinking) (husema kitu kilivyo.

iii)Hisia (Feeling) hizi huwa zinasema unakubali au la

iv)Machale (Intuition), hii inasema wakati wa kuja.

 

18.                      Umba ubongo wako uwe wa kiuwekezaji kama unataka kuwa mwekezaji bora na wa juu na uwe na ubongo wa (neuroeconomic)

 

19.                       Jifunze kuwa na wazo moja na lengo moja na huko mimina uwezo wako wote.

 

20.                      Goma kuishi Maisha ya ukawaida wewe si wakawaida nenda viwango vya juuu vya upekee wako.

Author

Contact Us

Name

Email *

Message *