SAFARI YA UTAJIRI NA NJIA ZAKE KUTOKA
KITABUNI
|
U
|
TAJIRI ni SAFARI inayopitishwa
katika hatua hizi 22 ambazo Mwandishi David Gikandi anaelezea kupitia
kitabu chake cha "A HAPPY POCKET FULL of MONEY"
Utajiri ni utambuzi wa fikra
kwanza kabla ya kupatikanika. Wale wanaotambua hili basi huanza na kubadili
kufikiri kwao kisha utajiri unaweza kuvutwa kirahisi. Fedha ni sehemu tu ya
aina za utajiri ambazo watu wengi wanajua. Lakini kuna aina za utajiri mbali na
fedha ambazo si wengi wana utambuzi huu. Karibu tuone hatua 22 za safari ya
kutambua utajiri na maisha ya furaha.
1.
Kwanza kabisa lazima utambue wale ambao wanaweza
kufanya makubwa maishani huwa wana utambuzi wa namna Dunia ifanyavyo kazi au
vitu vinavyofanya kazi. Kisha kwa kujua huko wanaendana na huo mfumo wa mambo
ulivyo. Utambuzi wa Dunia inavyofanya kazi ni maarifa makubwa ambayo yamefanya
watu wengi waje na ugunduzi, ubunifu na kutengeneza utajiri mkubwa tofauti na
wale wasio na utambuzi huo.
2.
Ufahamu wa muda unatenganisha watu katika kuyaelewa
maisha. Muda ni kiinimacho kwa watu wengi. Ukiondoa fikra basi umeondoa uwepo
wa muda. Hivyo muda pekee ambao ni halisi ni sasa. Kwa wanaopanga malengo basi
kwa kujua hili hupanga malengo yao kama yameshakuwa sasa.
3.
Maisha ni ujenzi wa picha akilini mwa mtu. Fikra
na hisia za mtu zinapoumba picha ndivyo mtu anavyovuta maisha yaliyo sawa na
picha anazoruhusu ziwe katika fikra zake.
4.
Kufikiri huzalisha mawazo na mawazo ni nguvu
yenye umbo. Mara ngapi jambo uliwaza halafu baada ya muda likatokea ?. Basi hii
ndiyo nguvu ya uvutano ya mawazo na kutokea kwa kitu katika umbo. Wenye
utambuzi huu hudhibiti mawazo yao wakijua mawazo ni maumbo yanayoweza kutokea.
5.
Watu wengi hawana ufahamu wa kina wa kupanga
malengo yanayoendana sawa na Dunia inavyofanya kazi na hivyo kujikuta hawapati
matokeo sawa na malengo yao. Wenye utambuzi wa kuyahusianisha malengo na
ulimwengu unavyofanya kazi basi huwa wanapata matokeo wanayoyataka.
6.
Ili uweze kuumba kitu lazima kwanza uruhusu uwe
( State of being ). Ili upate utajiri lazima kwanza ujione ndani yako utajiri
kisha uchukue hatua za malengo ya kukufanya uwe utajiri kisha upate utajiri kwa
kuuona katika umbo. ( Formula ni kuwa, kufanya na kupata ). Lazima upitie ( TO,
BE & HAVE ). Ila wengi hupuuza hii formula ndo maana kutengeneza maisha
mazuri au utajiri ni safari ngumu kwao.
7.
Bila kuchukua hatua huwezi kupata
ulichokifikiri. Kuchukua hatua ni kuruhusu kitu kiweze kutokea. Hata kama
utafikiri vizuri, utapata malengo vizuri na ukakosa kuchukua hatua hakuna
utakachokipata.
8.
Lazima uwe na utambuzi kuwa ulimwengu una utele
kuliko uhaba. Uhaba ni vile fikra zako zilivyo.
9.
Sheria ya asili ya kupanda na kuvuna kadri
unavyoweza kuitambua utakuwa unajua namna ya kutengeneza matokeo utakayo kwa
kuangalia upande nini ili uvune nini. Hii ni sheria mama ya kutengeneza utajiri
na maisha ambayo ungependa yawe kwa uzuri.
10.
Kuna watu hukosea pale wanapoangalia utajiri
kuwa una mazingira fulani pasipo kujua ni kitu kinachotengenezwa tokea ndani.
11.Mafanikio na kufeli ni pande
moja ya shilingi. Kufeli ndio njia ya kujua usahihi wa jambo na ukafanikiwa.
Wenye utambuzi huu basi huona kila hatua ya kufanikiwa kwao kufeli ni sehemu ya
mafanikio
12.
Kuna vitu ambavyo huangusha watu kuwa na utajiri
na furaha. Na hili lazima uliepuke ( ndani ya kitabu hiki tutajifunza namna ya
kufanya hivyo )
13.
Swali la nini kusudi la maisha yangu ? Nipo
naishi ili iweje ni muhimu sana kujiuliza. Kitabu hiki kimejibu vizuri kiasi
cha kushibisha kiu yako.
14.
Utoaji ni njia ya utajiri. Wenye utambuzi huu
wanajua ili ufanikiwe na kujifahamu wewe ulivyo basi kwa njia ya kujitoa
kuanzia vipaji, muda wako ndivyo utakavyoweza kujifahamu zaidi.
15.
Watu wengi wanadharau nguvu iliyopo katika
kushukuru. Kushukuru kuna Nguvu kubwa ya kuvuta maisha bora.
16.
Utambuzi ( Consciousness ) ndio kikwazo cha watu
wengi washindwe kupata baadhi ya vitu maishani hata kama vipo. Kadri unavyokua
ki utambuzi utaona Dunia ina utele na sio uhaba.
17.
Wewe ni mjenzi wa kwanza wa maisha ulonayo. Wewe
ni kisababishi cha matokeo unayoyapata nje. Kama hivyo maisha mazuri na mabaya
yapo kwako mtengenezaji.
18.
Kila kitu kinahusiana na vyote ni kama katika
umoja. Wale wanaojua hili basi wanatambua namna kwa jambo dogo linaweza kuumba
makubwa.
19.
Dunia ni tele na wewe ni sehemu ya utele. Ndani
yako kuna uwezo usioweza kupimwa ukaisha.
20.
Ili ufanikiwe na kuwa na furaha lazima urejee
katika asili yako na hapo ndipo chimbuko la furaha na utajiri wako.
21.
Fedha ni kiinimacho na ijue fedha halisi ni ipi
itakupa hatua za juu sana katika maisha.
22.
Unapojua haya basi wasaidie wengine kujua na
uwafundishe kujua ndivyo utajiri unavyoweza kusambaa kwa wengi.
Huu ni mwanzo wa safari ya
kitabu hiki. Hakika hutakuwa ulivyokuwa. Hebu chukulia uzito katika haya na
maisha yako hayatakuwa yalivyokuwa.